Sunday, March 31, 2013

Mandela aombewa afya njema

NELSON MANDELA MADIBA- SIMBA WA AFRICA, MFALME WA AMANI, BABA WA SOUTH AFRICA.

Makanisa ya Afrika Kusini yamemuombea rais mstaafu Nelson Mandela ambaye anatibiwa homa ya mapafu, pneumonia.

 
Waumini Afrika kUsini wakimuombea Mandela
Jumamosi msemaji wa Rais, Mac Maharaj, alieleza kuwa Bwana Mandela aliweza kuvuta pumzi bila ya shida na amepata nafuu, lakini bado wasi-wasi ungaliko kuhusu kiongozi huyo wa zamani wa Afrika Kusini mwenye umri wa miaka 94. Bwana Mandela aliishi mtaa wa Soweto, Johanneburg, kwa miaka mingi.
 
Mkaazi mmoja wa Soweto, Eddie Vilakazi, aliyemuombea Bwana Mandela katika ibada ya Pasaka Jumapili, anasema anatumai mzee huyo ataishi muda mrefu:
"Mandela ni kiongozi wetu.
Tunamuona kuwa mkombozi wetu.
Ni kila kitu kwetu.
Tunamtakia afya njema haraka.
Mungu amuangalie, ambariki kwa sababu tayari ameshabarikiwa.
Lakini tunamtakia maisha marefu zaidi, awe nasi."

THE WONDERS WE ARE PROUD OF...

 


FURAHA YA KILELENI HAIELEZEKI KARIBU, JARIBU TAFADHALI


Mount Kilimanjaro Overview

How High is Mount Kilimanjaro?

 

Mount Kilimanjaro is known to be the highest mountain peak in the continent of Africa. It is located in the northeast portion of Tanzania just close to the Kenya border. The mountain is actually an extinct volcano and one of the most enormous in our world. From the ground level, the mountain is towering for 15,000 feet above the encompassing dry plains. At the height of 18,500 feet, the surface area of the mountain is about two and a half square miles.
The total elevation of Mount Kilimanjaro is 19,563 feet or 5,963 meters. The best months to climb the mountain are January to March, June to August, and December. Below the ice dome of the mountain can be found the long gullies that extends down the mountainside due to snow erosions. The ice cap present on the mountain has been there for about 11,000 years ago but the size has decreased significantly these past years by as much as 80 percent. Scientists have expected the ice cap to be totally gone halfway through the 21st century.

Mount Kilimanjaro Craters

This enormous mountain in Africa has three volcanic cones called as Kibo, Mawenzi, and Shira, respectively. The summit crater of Mount Kilimanjaro is named as Kibo which has a measurement of one and a half miles across. The highest portion of Kibo’s rim is called as Uhuru and this is the highest peak all over Africa. At the center of Kibo lies a small crater full of sulfurous ashes that is 600 feet deep.
The second smaller cone of Mount Kilimanjaro is called as Mawenzi and has an elevation of 16,893 feet. Mawenzi ranks as the third highest peak in the African continent. Mawenzi is located about seven miles to the east of the cone Kibo and a long saddle has separated the two cones from each other. Mawenzi is an older cone that is already serrated from erosion exposing steep faces on various sides of the mountain. Even if the altitude of Mawenzi is much lower than Kibo, it is much more difficult to climb especially if you don’t have any skills with regards to snow and ice climbing as well as rock climbing.

Trekking the Mountain

Mount Kilimanjaro has five main trekking routes going to the summit and these are Marangu, Mweka, Shira, Machame, and Umbwe. The Marangu Route is the most famous of the five routes and commences at the elevation of 6,000 feet at the Marangu Gate. The trekking route has available facilities and huts for the climbers along the way. The rest of the trekking routes have more excellent views and stunning scenes of the glaciers on the mountainside. These routes are good for the advanced climber because the trail is more challenging and a special permit must be acquired first before you can pursue the course.

DO WE HAVE LEADERS? ARE YOU A GOOD LEADER?: ARE YOU SURE THAT YOUR A GOOD LEADER?


THE BANK THAT LISTENS




RAIS KIKWETE NA MKEWE MAMA SALMA KIKWETE WATEMBELEA WAHANGA WA POROMOKO LA GHOROFA DAR ES SALAAM NA KUWAPA POLE.



Raisi Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakimpa pole mojawapo wa majeruhi bwana Yusuph Abdallah.


ARE YOU THE CHANGE?


BE THE CHANGE WE/YOU DESIRE


Sunday, March 24, 2013

HUGO CHAVEZ............



HUGO CHAVES RAFAEL FRIAS
 
Iilikuwa ni  safari nyingine ya kuelekea miaka sita kwa kiongozi huyu wa Venezuela aliyedaiwa  kuwa misimamo isiyoterere

Rafiki wa wa watu  maskini ,pamoja na jitihada zake za kuikomboa nchi ya Venezuela ,kifikra na vilevile kiuchumi adui maradhi naye hakuwa mbali kwa kiongozi huyo.

Ugonjwa wa Saratani  uliendelea kuodhoofisha afya yake licha ya jitihada zilizofanywa kuutokomeza ugonjwa huo.

 Hugo Rafael Chavez Frias alizaliwa Julai 28, 1954. Alishika madaraka ya kuiongoza Venezuela tangu mwaka 1999.

Kufuatia itikadi yake ya kisiasa ya Kibolivarian na "Usoshalisti wa karne ya 21", alilenga katika kutekeleza mageuzi ya usoshalisti katika nchi kama sehemu ya mradi wa kijamii inayojulikana kama Mapinduzi ya Wabolivia, ambayo yameshuhudia utekelezaji mpya wa katiba, demokrasia shirikishi na kutaifisha viwanda kadhaa muhimu.

Hugo Rafael Chavez Alizaliwa Sabaneta, Barinas, akawa afisa kazi jeshini, na baada ya kutoridhika na mfumo wa siasa za Venezuela ambao aliuona kama wa rushwa na sio wakidemokrasia, alianzisha Vuguvugu la siri la Mapinduzi ya Kibolivarian-200 (MBR-200) katika miaka ya 1980 ili kuipindua serikali.



Baada ya tukio hilo ,serikali ya Rais Carlos Perez Andres aliamuru ukandamizaji mkali wa maandamano dhidi ya kupunguzwa matumizi,yaliongozwa na Chaves

Katika mapinduzi yaliyoshindwa dhidi ya serikali mwaka 1992, rais Chaves  aliishia kufungwa jela.

Alipotoka gerezani baada ya miaka miwili, alianzisha chama cha siasa, Fifth Republic Movement, na alichaguliwa kuwa rais wa Venezuela mwaka 1998.

 Hatimaye alipendekeza katiba mpya ambayo iliongeza haki kwa makundi yaliyotengwa na ilibadilisha utaratibu wa serikali ya Venezuela, hali iliyomfaya arudie tena madarakani  mwaka 2000.
 
Wakati wa muhula wake wa pili wa urais, alianzisha mfumo wa Misheni ya Kibolivarian, Halmashauri za Kijamii na vyama vya ushirika vinavyosimamiwa na wafanyakazi, wakati pia alitaifisha viwanda mbalimbali muhimu kwa maslahi ya taifa.

Wapinzani wakati huohuo, walionesha hofu kwamba alikuwa akiumomonyoa uwakilishi wa kidemokrasia na kujiongezea mamlaka, ambapo walijaribu kumwondoa madarakani kwa njia zote kupitia mapinduzi ya kijeshi yaliyoshindwa mwaka 2002 na kura ya maoni ya mwaka 2003.
 

Alichaguliwa tena mwaka 2006, kufuatia kuanzisha chama kipya cha siasa, United Socialist Party of Venezuela (PSUV), mwaka 2007.

alijulikana kama mkosoaji wa ubepari na hasa uliberali wa kisasa, Chávez amekuwa mpinzani maarufu wa sera za kigeni za Marekani.

 Akifungamana mwenyewe na serikali ya ujamaa ya Fidel na kisha Raul Castrol ya Cuba, ya Evo Morales wa Bolivia, na ya Rafael Correa wa Ecuador.

Urais wake unaonekana kama sehemu ya “mrengo wa kushoto” ukiisafisha Amerika ya Kusini.

Amekuwa anaunga mkono ushirikiano wa Amerika Kusini na Caribbean na alikuwa mtu muhimu katika kuanzisha ushirikiano wa kanda nzima; Umoja wa Mataifa ya Amerika Kusini, Muungano wa Wabolivia kwa ajili ya Waamerika, Benki Kuu ya Kusini, na mtandao wa televisheni wa kikanda, TeleSur.

Ushawishi wake wa kisiasa katika Amerika ya Kusini ulimfanya jarida la Time kumuweka katika orodha ya watu 100 wenye ushawishi mkubwa zaidi duniani katika miaka ya 2005 na 2006.



Hugo Chávez amefariki dunia  kwa ugonjwa wa saratani akiwa na umri wa miaka hamsini na nne

Saturday, March 23, 2013

MIKADI BEACH, ENEO LAKO LA KUTEMBELEA



Unapozungumzia suala sehemu binadamu kuwepo kitu cha kwanza kuangalia ni suala la usalama kasha mambo mengine hufuata
                Binadamu anahitaji kuwa salama na ndio maana mtu yeyote anapotaka kutembelea mahali popote kitu cha kwanza kuulizia ni suala la usalama awe mwenye mtanzania  au mtu mgeni toka nje ya Tanzania               
                Kwa wiki hii tunaangazia eneo la kupumzika hapa Dar es Salaam liitwalo Mikadi Beach lipatikanalo Kigamboni
Hii ni beach iliyojihakikishia usalama wa hali ya juu na huduma mbali mbali za kibinadamu kwa umakini wa hali ya juu
                Akizungumza na NIHABARISHE meneja wa Mikadi beach bwana Fransis Raphael amesema kuwa beach hiyo imejitosheleza kila kitu kwa malazi chakula na starehe za aina mbalimbali kama kuogelea na burudani mbalimbali
                ‘’Suala la usalama wa mtu ni muhimu sana na ndio maana sisi tuna ulinzi wa kiteknolojia na wa binadamu manake mteja akiwa hapa na kupata tatizo hawezi kuja tena na hawezi kufahia kuwepo hapa, tunapokea wageni wa aina mbalimbali na ndio maana wafanyakazi wetu ni wa kutoka nchi mbalimbali’’
                Mikadi  tangu kuanzishwa kwake na kuchukuliwa na wamiliki wa sasa mwaka 2008 pamekuwa na kimbilio la watu wa aina mbalimbali tokana na huduma zake
                Kwa mujibu wa Bwana Francis Raphael Mikadi inaweza kuhudumia zaidi ya watu 150 kwa siku moja.
                Mikadi imekuwa ni eneo ambalo watu mbalimbali toka ndani na nje ya nchi hufanya harusi zao na kupata huduma safi
                Kutokana na kasi ya maendeleo ya sayansi na teknolojia Mikadi nao hawako nyuma kutokana na kuboresha huduma za kuwasiliana na wateja wao kisasa zaidi kupitia mtandao ambao wa www.mikadibeach.com ambao upo tayari kila wakati kubadilishana mawazo na watu wahitajio huduma mahali pale

               


PROF. CHINUA ACHEBE AAGA DUNIA

 
Albert Chínụ̀á  lụmọ̀gụ̀ Àchèbé  mwandishi mkongwe barani afrika ,alizaliwa  tarehe  16 Novemba 1930) katika mji wa Igbo  kijiji cha  Ogidi  kilichopo kusini mashaririki mwa nchini  hiyo, Ni mwandishi wa vitabu mbalimbali Barani Afrika na dunia kwa ujumla  akitokea  nchi ya Nigeria
Ameandika vitabu vingi vyenye riwaya, mashairi na insha, Hadithi zake zinazotumika hadi sasa zinatumia mitindo ya fasihi simulizi ya lugha yake ya asili, Kiigbo. Hata hivyo ameandika hasa kwa Kiingereza. Baadhi ya maandiko yake ni pamoja
Mwaka 1958, aliandika kitabu kilichovunja rekodi kwa kuuza nakala milioni kumi sehemu mbalimbali ulimwenguni akakiita  "Things Fall Apart baadaye vikafuata vitabu vingine lukuki vikiwemo
mwaka 1960, "No Longer At Ease’
mwaka1964,  "Arrow of God"
mwaka 1973,  "Girls at War")
·         Shida na Nigeria (mwaka 1984, kwa Kiingereza "The Trouble with Nigeria")
·         (mwaka 1987, kwa Kiingereza "Anthills of the Savannah")
·         Picha ya Afrika (mwaka 2000, kwa Kijerumani "Ein Bild von Afrika")
 Isaiah Okafo Achebe na Janet Anaenechi Iloegbunam  wazazi wa mwandishi huyu  waliishi maisha maisha ya kitamaduni yaliyokuwa na ukristo ndani yake ambayo yanatajwa kumsaidia motto wao Chinua Achebe.
Baada ya  mdogo wake kuzaliwa ,familia yake  ilihamia katika mji wa Anambra sehemu ambako ndiko zilikokuwa  mila na tamaduni za kiigbo
Akiwa na umri mdogo mama yake pamoja na dada yake  Zinobia Uzoma  walipenda  sana kumwadithia  hadithi mbalimbali zilizohusu maisha ya mila na\  tamaduni tamaduni zao
Mwaka  1936, Achebe  alianza elimu yake ya msingi  katika shule ya kati ya  St Philips' ambapo  pamoja na kuwapo kwa maandamano wa kati huo , alitumia  muda wake mwingi  katika kupata elimu  ya kidini  ambapo alionekana kuwa na uelewa mkubwa zaidi hali iliyomsaidia kupanda kidarasa kwa haraka zaidi.
Chinua alipendwa sana na Walimu wake  ambapo mmoja   aliweka  wazi kwamba  ni mwanafunzi pekee aliyekuwa na mwandiko mzuri darasani  pamoja  ujuzi mkubwa wa kusoma zaidi.
   Pia  alikuwa akihudhuria  shule ya jumapili  kila  wiki  pamoja na huduma maalumu ya  kiinjilisti  zilizokuwa ziktolewa killa mwezi huku akiwa na mkoba wa baba yake
Akiwa na umri wa miaka kumi na mbili Achebe  aliondoka nyumbani kwao na kuelekea katika kijiji cha  Nekede kilometer nne ukitokea mji wa owerri na kujiunga  na shule ya kati ambayo kaka yake alikuwa akifundisha.
Katika mji wa  Nekede  alipata kutathimini  mila na tamaduni za kimbari ambao ulikuwa umejikita zaidi katika kuabudu miungu pamoja na utoaji wa sadaka .
Mwaka 1944 muda ulifika kwa Achebe kubadili shule ya sekondari ambapo alipewa mtihani na kufanikiwa  kujiunga  na  shule ya kifahari ya Dennis Memorial Grammar School  iliyoko katika mji wa Otisha pamoja na chuo cha serikali  kwenye mji wa U muahia  
Shule  hiyo ilianzoishwa na watawala ukoloni wa waingereza  ambapo pia chuo hicho cha serikali kilianzishwa 1929 kuwaelimisha wasomi wajao wa NIGERIA. Kiwango cha taaluma kilikuwa ncha juu sana ,wanaume walipewa kipao mbele huku lugha iliyotumika kufundishia ikiwa ni Kiingereza
Kutokana na uelewa mkubwa aliokuwa nao   katika shule  hiyo ya sekondari  ndani ya mwaka mmoja alisoma madarasa mawili  na hivyo kumfanya ahitimu  kwa miaka mine, elimu ya sekondari badala ya miaka mitano
Achebe  kwa wakati huo hakupendelea sana michezo iliyokuwa ikichezwa na wanafunzi wenginebadala yake.
Alifanya upelelezi katika maktaba kubwa iliyokuwa shuleni hapo na kugundua kupo kwa vitabu vya historia pamoja na riwaya mbali mbali ambazo alizisoma.
Mwaka 1948, katika maandalizi ya uhuru wan chi ya Nigeria ,Chuo kikuu kipya kilianzishwa ambacho kwa sasa kinaitwa Chuo kikuu Cha Ibadan,  kwa wakati huo kilishirikiana  na Chuo Kikuu Cha London
Achebe alipata alama za juu katika mtihani wa kujiunga na chuo hicho na kufanikiwa kupata nafasi  ya kusoma bure katika chuo ambapo kwa mwaka wa kwanza akapata msaada wa fedha  akisomea udaktari
Baada ya mwaka mmoja  alibadili kozi hiyo ,nakuchukua  masomo mengine  ambayo ni Kiingereza ,Historia na theolojia ambapo baada ya kubadili alipoteza nafasi ya kusomeshwa bure na alilazimika kulipia masomo yake ya ziada
Baadaye serikali ilimpatia fedha kidogo  ambazo hazikutosheleza ambapo pia   chinua alilazimika kuchangisha fedha katika familia yake na pia kwa  kaka yake aliyekuwa akifanya kazi serikalini alimchangia ili asikatishwe masomo yake
Chuo kikuu kipya cha Ibadan  kilikuwa na kitivo makini cha Lugha  ya Kingereza   pamoja na  waathiri mashuhuri ambao pia ni waandishi wa vitabu  ka vile Nobel Laureate Wole Soyinka,,Elechi Amadi, John Pepper Clark na Christopher Okigbo.[26]
Katika miaka , 1950 angali bado chuo kikuu  alianza  kuandika   stori fupi ambapo story yake ya kwanza ilikuwa ni  In a Village Church" ikijumuisha    ya  watu waliko vijijini  pamoja na taasisi za dini ya kikristo  Nyingine zilizofuta   "The Old Order in Conflict with the New" and "Dead Men's Path"  zikielezea vita kati utamadu  na maisha ya usasa
Baada ya kuwasili  kwa  professor   Geoffrey Parrinder  katika  chuo cha Ibadan  kufundisha  Ushirikiano wa kidini , Achebe  alianza kupeleleza  juu ya chimbuko la dini ya kikristo na tamaduni za afrika.
Mwaka 1953,  achebe alifanya mt ihani wake wa mwisho  wa shahada yake ya kwanza katika chuo kiku cha  Ibadan  na   kufaulu  katika daraja la pili ambpo alirejea nyumban  kwao  Ogidi kuoangalia machagu yake.
Baada  kuhitimu elimu yake alifundisha lugha ya kiingereza katika shule ya biashaRA  Oba AMBAPO 1954 akaanza kufanya  kazi na Shirika la utangazaji La Nigeria NbC NA KUAHAMIA  LAGOS. Alifanya shughuli nyingi akiwa na shirika hili.
Katika vita vya Biafra  1967  iliyotaka kujitenn nga kwa jimbo  la Biafra Achebe  aliunga mkono vita hivyo ,alitumikia kama balozi wa watu wa taifa jipya la Biafra  ,Baadaye serikali ilishinda NA Kuchukuwa utawala wa jimbo hilo huku CHINUA kuwaombea msaada watu wa lililokuwa taifa lake.
Baada ya utawala wa Nigeria kulichukuwa jimbo hilo 1970 aliamua kuwa mwanasiasa lakini baadaye alijiuzulu kutokana kuwapo kwa mpasuko uliosababishwa na rushwa kwa uliokuwa kwa wasomi wakati huo
Katika miaka ya 1970 Chinua aliishi nchini Marekani kwa miaka mingi Ambapo 1990 alihamishia makazi  ya kudumu nchini humo baada ya kupata ajali ya gari iliyomsababishia ulemavu wa miguu
tangu mwaka 2009 mpaka mauti ilipomkuta  2amekuwa professa wa masomo ya kiafrika katika chuo kiku cha Brown  kilichopo nchini Marekani


PINDA NA MKEWE WAMTEMBELEA PAPA MPYA

Waziri mkuu mheshimiwa Mizengo Pitter Kayanza Pinda na mkewe Mama Tunu Pinda wamemtembelea papa mpya huko mjini Vatican Roma nchini ITALY
Waziri mkuu na mkewe mbali na kuonana na Papa Francis 1 walipata nafasi ya kupata historia ya mji wa Vatican, pia walipata interview na redio moja huko Vatican.
Viongozi kadha wa kadha kutoka barani Africa wamemtembelea papa mpya akiwemo rais wa Zimbambwe Robert Mugabe