Saturday, March 23, 2013

MIKADI BEACH, ENEO LAKO LA KUTEMBELEA



Unapozungumzia suala sehemu binadamu kuwepo kitu cha kwanza kuangalia ni suala la usalama kasha mambo mengine hufuata
                Binadamu anahitaji kuwa salama na ndio maana mtu yeyote anapotaka kutembelea mahali popote kitu cha kwanza kuulizia ni suala la usalama awe mwenye mtanzania  au mtu mgeni toka nje ya Tanzania               
                Kwa wiki hii tunaangazia eneo la kupumzika hapa Dar es Salaam liitwalo Mikadi Beach lipatikanalo Kigamboni
Hii ni beach iliyojihakikishia usalama wa hali ya juu na huduma mbali mbali za kibinadamu kwa umakini wa hali ya juu
                Akizungumza na NIHABARISHE meneja wa Mikadi beach bwana Fransis Raphael amesema kuwa beach hiyo imejitosheleza kila kitu kwa malazi chakula na starehe za aina mbalimbali kama kuogelea na burudani mbalimbali
                ‘’Suala la usalama wa mtu ni muhimu sana na ndio maana sisi tuna ulinzi wa kiteknolojia na wa binadamu manake mteja akiwa hapa na kupata tatizo hawezi kuja tena na hawezi kufahia kuwepo hapa, tunapokea wageni wa aina mbalimbali na ndio maana wafanyakazi wetu ni wa kutoka nchi mbalimbali’’
                Mikadi  tangu kuanzishwa kwake na kuchukuliwa na wamiliki wa sasa mwaka 2008 pamekuwa na kimbilio la watu wa aina mbalimbali tokana na huduma zake
                Kwa mujibu wa Bwana Francis Raphael Mikadi inaweza kuhudumia zaidi ya watu 150 kwa siku moja.
                Mikadi imekuwa ni eneo ambalo watu mbalimbali toka ndani na nje ya nchi hufanya harusi zao na kupata huduma safi
                Kutokana na kasi ya maendeleo ya sayansi na teknolojia Mikadi nao hawako nyuma kutokana na kuboresha huduma za kuwasiliana na wateja wao kisasa zaidi kupitia mtandao ambao wa www.mikadibeach.com ambao upo tayari kila wakati kubadilishana mawazo na watu wahitajio huduma mahali pale

               


No comments:

Post a Comment