Sunday, February 3, 2013

DC BAGAMOYO BALAA , ANAKUBALIKA NA WAMKUBALI, WASHIRIKI WAIMBA WIMBO KUWA NA IMANI NAYE 100%:




DC Bagamoyo, Ndugu Ahamed Kipozi awasisitiza vijana wa Bagamoyo kuutumia vema Ujana wao
Na Adam Ngamba
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ndugu Ahmed Kipozi amewasisitiza baadhi ya vijana walioshiriki mafunzo ya Ujasiriamali na UKIMWI yaliyofanyika katika hoteli ya SKY READ  kwa muda wa wiki moja ambayo yaliwahusisha vijana wasio na kazi maalumu, wahudumu wa baa, watumia ma ndawa ya kulevya pamoja na wa wafanya biashara wa kuhamahama.

Hayo ameyaseme wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya Ujasiriamali na UKIMWI yaliyo fanyika, kuanzia tarehe 28 Januari-1, Februari 2013.
Mafunzo hayo ambayo yalikuwa yakitolewa na wataalamu mbalimbali chini ya Usimamizi wa Asasi ya Uwezeshaji Tanzania (ASUTA) na Progress the Youth Foundation zilizo chini ya udhamini mfuko wa RAPID FUND ENVELOPE (RFE); yameonekana kupokelewa  kwa furaha na Mkuu wa Wilaya  pamoja na  vijana walioshiriki mafunzo hayo.
Katika hutuba yake fupi iliyotumia yapata dakika 20, Ndugu Kipozi amewasisitiza vijana kuchangamkia fursa ya kujifunza angali bado damu inachemka na wakati  wakiwa na nguvu za kufanya kazi barabara.
“ ………Katika maisha kuna hatua tatu muhimu; hatua ya utoto, ujana na utu uzima. Kila hatua inasifa na wakati wake. Lakini hatua muhimu zaidi katika maisha ni hii ya ya pili ya ujana ambapo kijana anakuwa bado na nguvu zake zote. Na hii ndiyo hatua ya kijana kuwa na juhudi kubwa katika kutafuta maendeleo endelevu kwani ni hatua hii ndiyo inayotoa muelekeo wa maisha na ndiyo maana ikapewa majina mengi kama vile ‘ujana maji ya moto’ damu inachemka na kazalika………”
Aidha Ndugu Kipozi aliwaeleza washiriki wa mafunzo hayo kuwa maendeleo hayawezi kuja kama mvua, bali ni kwa kuzingatia mambo muhimu matatu; nia au malengo, bidii na juhudi katika kazi na maarifa ama ujuzi katika kufanya kazi kwa ufanisi zaidi ili kufikia malengo.
Ndugu Ahammed Kipozi hakusita kuidhihirisha furaha yake kwa kuipongeza ASUTA na PY na uongozi mzima wa Asasis hiyo kwa kuonesha nia njema ya kuiunga mkono serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika kutekeleza sera yake ya  kupunguza umasikini uliyokithiri na kuunda ajira kwa vijana na jamii nzima ya Kitanzania.
Mkuu huyo wa wilaya ya Bagamoyo, aliongeza pongezi zake kwa ASUTA na PY kwa kutokusahau kutoa mafunzo dhidi ya maambukizi ya VVU/AIDS na  maradhi mengine yanayo weza kuenezwa kwa njia ya ngono isiyo salama.  
Ndugu Kipozi alisema kuwa ni muhimu sana kwa jamii hasa vijana kujifunza masuala ya afya kwani afya ndiyo kila kitu, kwa kuwa mtu hauwezi kuelezea maendeleo ya jamii bila kuzungumzia afya.
Mbali na hapo, Ndugu Kipozi amewasisitiza vijana kushiriki kwa wingi pindi fursa kama hizi zinapojitokeza kwani mtu hawezi kujifunza akiwa kajifungia ndani tu, ni lazima ajichanganye na wenzie na kuonesha ushirikiano wa hali na mali. Na ili kukamilsha adhima hii, mkuu huyo ameushauri uongonzi wa ASUTA na PY kutumia mfumo jumuishi wa mawazo, ikiwa ni pamoja na kupokea ushauri ama mawazo kutoka kwa washiriki wengine na kuwashirikisha katika mipango mbalimbali ya kimaendeleo.
Katika muendelezo wa habari, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ndugu Kipozi aliendesha zoezi la ugawaji wa baiskeli takribani 20 kwa baadhi ya waelimishaji rika, ambazo zilitolewa na ASUTA na PY kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa maendeleo unao simamiwa na Asasi hiyo yenye ofisi zake hapo mjini Bagamoyo.





No comments:

Post a Comment