Monday, February 11, 2013

FOUNDATIN FOR CIVIL SOCIETY YAFANYA MAFUNZO YA KUJENGEA UWEZO AZAKI.


Washiriki wa mafunzo ndani ya THE NEW DODOMA HOTEL.

Shirika lisilokuwa la kiserikali Foundation for civil Society FCS leo limenza kutoa mafunzo kwa Asasi Zisizo za Kirai (AZAKI) mjini DODOMA katika hoteli ya THE NEW DODOMA HOTEL. Kutokana na vyanzo vya habari vya nihabarishe mafunzo hayo yatadumu kwa siku tano kuanzia 11/02/2013-15/02/2013.
Foundatio For Civil Society ni shirika ambalo liko mstari wa mbele kuhakikisha kuwa NGO/AZAKI zinatimiza malengo yake kwa ajili ya kusaidia jamii kukabiliana na matatizo mbalimbali yakiwemo umaskini uliokithiri, kurekebisha sera butu, ushawishi wa sera na utawala bora
Kwa upande wao  washiriki wa mafunzo hayo toka sehemu mbalimbali za Tanzania wameshukuru sana kwa mafunzo hayo kuwaondoa katika giza
“Kwa mara  ya kwanza nimefurahia kuhudhuria mafunzo ya Foundation for Civil Society kwani ni dhahiri nilikuwa sijui umuhimu wa hati ya malipo katika shirika letu leo hii nimejua nasikujua kuandaa mchanganuo wa mapato na matumizi lakini leo kupitia mwalimu wa mafunzo Bwana Tuntufye Mwaiteleke nimeyajua hayo” alisema Sister Aneth Mwani toka Emau Development toka Njombe.

Sister Aneth Mwani akipoza kwa picha mara baada ya mafunzo hayo.

Aidha mshiriki mwingine bwana Godwin Maganga toka TUMAINI DISABLED COMMUNITY toka Tabata Dar es Salaam alisema nae kafurahi pia kwa yote yaliyofundishwa juu ya mchanganua wa fedha ndani ya asasi. 

Bwana Godwin Manganga akiwa amepozo kwa picha mbele kidogo ya lango la THE NEW DODOMA HOTEL



Kwa upande wake mwezeshaji wa Semina hiyo Bwana Tuntufye Mwaitekele alijikita kwenye mada za Usimamizi wa fedha, Udhibiti wa Fedha na nguzo zake kama Muundo, Muungozo na Mfumo, aliweka bayana viashiria vya muundo madhubuti ili kuwezesha AZAKI kuleta tija katika utekelezaji wa miradi. Pia washiriki wamewezeshwa kujua jinsi ya kuandaa Mchanganuo wa Mapato na Matumizi ya fedha katika shirika na umuhim wake. Kingine cha msingi Mwezeshaji aliweka bayana utenganisho wa Majukumu ndani ya Asasi hapa ndipo maswali mengi yalimiminika toka kwa washiriki lakini kutokana na uzoefu wa mwezesha bwana Tuntufye L. Mwaitekele aliwajibu na kuwaelewesha vizuri alitumia ueledi wa juu na mbinu shrikishi mpaka mwisho wa siku washiriki waliokuwa na maswali wameelewa hii ni kutokana na vyanzo vya habari vya NIHABARISHE na uchunguzi wa kina uliofanywa na NIHABARISHE kwa njia ya focus group discussion na mahojiano ya mtu kwa mtu (Oral Interview).


 Washiriki wakiwa ndani ya ukumbi wa THE NEW DODOMA HOTEL.

No comments:

Post a Comment