Monday, December 17, 2012

MAPINDUZI YA BLOG YAJA NA KAULI MPYA



ISAPOTI, IPENDE......


 KAULI YA MWENYEKITI MTENDAJI.
Tanzani ni kati ya nchi mojawapo zilizokumbwa na mtikisiko au anguko kubwa la uchumi zikiwemo bei za vitu kupanda bila kukoma na huku huduma za kijamii zikizorota. Kadhalika serikali pamoja na sekta binafisi kuwa zimefinywa na upepo huu mgumu kushindwa kupanua ajira zinazoweza kukidhi mahitaji ya vijana wengi wanaozalishwa na vyuo kila kukicha.
Hii imesababisha hali ya vijana kuwa mbaya kila kukicha kutokana na kuhitimi elimu ya juu na kukosa ajira. Vijana wamekuwa katika msongo wa mawazo wengi wao kujiingiza kwenye shughuli hatarishi katika maisha yao zikiwemo ulevi ulokithiri, utoaji mimba, umalaya, uuzaji madawa ya kulevya, wizi na cha kushangaza zaidi, jinsia isiyotegemewa kufanya biashara ya Ngono nayo imeanza kwa kasi hawa si wengine ni vijana wetu wa kiume kujiuza kwa majimama yenye fedha yawalee au kuwaweka sawa hapa mjini Dar Es Salaaam na miji mingine. Hii imesabababishwa na kukosa matumaini ya maisha kutokana na ukosefu wa kazi baada ya kuhitimu masomo wakati Sera ya habari inawalinda, sera ya Vijana inawalinda na Sera ya Uwekezaji inawalinda:
NIHABARISHE inaleta sura mpya na suruhu ya haya matatizo lisapoti lipende na 10% inachangiwa kwa watoto wanaaoishi mazingira hatarishi ambao pia ni matokeo ya haya matatizo.
NIHABARISHE litatoa kipaumbele kuajiri na kushirikisha moja kwa moja vijana wenye ueled kupata ajira.
Aidha litaonya na kufundisha maadili kufuatwa hata kama ugum wa miasha umekithiri kwani suluhu huwa ipo tu pindi nguvu zinapounganishwa kwa pamoja yaani, serikali, watu binafsi, mashirika mbalimbali kwa pamoja tunaweza kufanya changamoto kuwa fursa zinazong’aa na si kumcha mheshimiwa Raisi au kikundi Fulani tu kutetea jambo hii. Tukisoma sera zetu vizuri tutweza kufanisha haya yote, kwa pamoja tunaweza
Prince Pastory

No comments:

Post a Comment