Wednesday, December 26, 2012

TAMRA YATOA ONYO

 
TAMRA YAONYA WANAUME WAZINGATIE SHERIA ZA NCHI VINGINEVYO WANAUME WAKOROFI HAITAWASAIDIA
Na - SELEMANI PHARLES MABALA - DAR ES SALAAM
Chama cha kutetea haki za Wanaume Tanzania TAMRA kimewataka Wanaume kote nchini kuzingatia sheria za nchi na kuacha mara moja kuonyesha ubabe kwa kujichukulia sheria mkononi kwa kuwapiga wanawake wakati wakiwa wametenda makosa mbalimbali majumbani mwao vinginevyo hakitakuwa tayari kumlinda mwanaume yeyote ambaye atakuwa amekwenda kinyume na matakwa ya chama hicho.
Kauli hiyo imetolewa na viongozi wa chama hicho nchini akiwemo mwenyekiti wa chama hicho nchini Bwana Belensi Alkadi na  Katibu Mkuu wa chama hicho nchini Bwana Antony Sollo walipokuwa wakizungumzia hoja mbalimbali pamoja na changamoto zinazowakabili wanaume mbalimbali nchini.
Bwana Sollo amesema wanaume hukumbana na matatizo makubwa katika familia zao lakini hakuna namna nyingine itakayosaidia kuidumisha amani ndani ya familia hizi isipokuwa wanahitaji kuwa wavumilivu,na zaidi ya yote watumie busara zaidi,hekima zaidi katika kuyamaliza masuala mbalimbali na changamoto za wanandoa kwa vile hakuna kitu kinachomkuta mwanandoa kwa bahati mbaya bali hatua ya kwanza ni kukumbuka kuwa wanandoa hawa waliapa viapo vya utii kwa mungu wao siku ya ndoa yao viapo hivi vinakwenda sambamba na uvumilivu katika mambo mbalimbali ikiwemo umaskini,utajiri, magonjwa na mambo mengine ya aina hiyo ambapo bwana Sollo ameshangazwa na tabia ya mmoja wa wanandoa kufikia kumlalamikia mwenzake kuwa ameshindwa kuvumilia shida za mwenzake na kwa sasa hana uwezo tena wa kuendelea kuishi na mtu ambaye hawezi kumtunza na kuamua kuivunja ndoa bila ya kuwashirikisha hata viongozi wa dini pamoja nan wazazi ambao ni mojawapo wa waliobariki na kutoa kibali cha wawili hawa kuishi kama mme na mke.
Naye Mwnyekiti wa chama hicho nchini akizungumzia hali ya mifarakano ya kifamilia amesema kuwa moja ya vitu vinavyochangia kwa kiasi kikubwa kutokea kwa matatizo katika ndoa na kupelekea kuongezeka kwa idadi ya watoto wa mitaani ni pamoja na mmomonyoko wa maadili ya Mtanzania kwa vile baadhi ya familia zimekuwa na majukumu ya kujitafutia maisha huku zikiwaachia watumishi kulea watoto bila kushiriki kwa wazazi kufundisha malezi bora kwa watoto,maendeleo ya Sayansi na teknolojia kwa vile kwa sasa watoto hujua haraka mambo makubwa ambayo umri ulikuwa haujafikia kuyajua na kuyatenda  jambo linalosababisha kupungua kwa kasi kubwa kwa heshima katika jamii.
 Akizungumzia malezi na makuzi ya kipindi kilichopita Bwana Sollo amesema kuwa zamani watu walikuwa hawawezi kuzungumza juu ya mambo ya mahusiano ya kindoa tofauti na ilivyo sasa ambapo tafiti zinaonyesha kuwa watoto wengi kuanzia shule za msingi na sekondari huanza mahusiano ya kimapenzi mapema na matokeo yake kushusha kiwango cha Elimu kwa kuwa mapenzi na shule ni sawa na kulima huku ukishindwa kupalilia na hatimaye kwa sababu ya kujitetea tu mtu anasema kuwa kuna uchawi umefanyika na kupelekea kushindwa kwake kuvuna mazao.
Hata hivyo akizungumzia changamoto walizo nazo wanandoa hasa wa kiume ni juu ya umaskini na hata kipato, kwa vile kwa sasa baadhi ya wanaume wamekuwa wakipambana na matatizo makubwa baada ya kushindwa kumudu maisha kufuatana na changamoto zinazowakabili ikiwamo kukosa kipato, ugonjwa sugu kama mabusha matende,Ukimwi HIV/AIDS na mambo mengine kama hayo.
TAMRA Imejipanga kukabiliana na changamoto hizi kwa kutoa elimu kwa mwanaume wa Tanzania pamoja na mototo kiume ili kuondoa dhana ya mfumo dume katika kuweka haki sawa kwa wote,amewaomba wanaume kuwa na subira na kuacha kujichukuliasheria mkononi kwa vile endapo watatenda mambo yaliyo kinyume na malengo ya chama hiki hawatakuwa tayari kuwatetea wanaume ambao watakiuka haki za binadamu kwa vile watakuwa wamevunja kanuni taratibu sheria pamoja na katiba inayoongoza nchi.
Nikweli yapo mambo yanayofanyika kwa uonevu lakini TAMRA iko macho sana kulinda na kutetea haki sawa kwa wote kwa vile siku ya Alhamisi wiki hii Katibu mkuu baada ya kuhojiwa na kituo cha ITV aliacha namba za mawasiliano na hatimaye alipigiwa simu kutoka Mkoa wa Geita ambako alipewa taarifa ya mtu mmoja ambaye alikuwa chini ya ulinzi wa sungusungu kwa masaa kadhaa akisubiri kusurubishwa na alipopata wasaa wa kwenda kujisaidia tu aliomba msaada wa simu na kupata nafasi ya kuongea  na katibu Mkuu wa TAMRA Bwana Antony Sollo ambapo Katibu huyo baada ya kupata maelezo aligundua ukiukwaji wa haki za binadamu na hivyo  aliwaagiza sungusungu hao kumuachia mkara moja Bwana Malimi mkaazi wa Kabuhima Runzewe Mkoani Geita na baada ya hapo walitoa taarifa kuwa tayari Bwana Malimi yuko nje na hivyo suala lake litafikishwa panapohusika.
Akielezea tukio hilo Katibu Mkuu wa TAMRA anasema, ilikuwa saa kumi jioni nilipigiwa simu na mtu mmoja aliyejitambulisha kuwa yeye ni Bwana Malimi kutoka kijiji cha Kabuhima  Runzewe Mkoani Geita ambapo yeye alikuwa ameenda kwenye mihangaiko yake tangu asubuhi ,cha kushangaza aliporudi tu alimkuta mke wake amelewa chakali na watoto wake hawajala chakula tangu asubuhi na alipouliza kulikoni akajibiwa kuwa mimi9 siyo House Girl wa familia hiyo na kama anaona vipi aende kutafuta House Girl atakayekuwa mtu wa kuhudumia familia hiyo jambo lililomfanya agadhabike na kumpiga kofi mke wake na baada ya muda mfupi mama huyo alipiga simu mara walitokea watu walikuja na kumkamata Bwana Malimi na kumpeleka ofisi ya sungusungu na kumuweka chini ya ulinzi  ambapo mwenyekiti wa sungusungu aliomba watoe fedha kwa ajili ya kusikilizwa kwa kesi yao ambapo mama huyo alitoa shilingi elfu themanini papo kwa papo huku akimuacha hoi mmewe kwa vile alikuwa hajui fedha hizo mkewe alizitoa wapi na hivyo alishinikiza akae rumande hadi siku inayofuata ambapo baada ya kituo cha ITV kurusha moja kwa moja mahojiano na Katibu Mkuu wa chama hicho ndiko kulipelekea ukombozi wa Bwana Malimi na Amewataka wanaume kote nchini kukiunga mkono na kukiamini chama hiki kuwa ni ukombozi wa mwanaume na ni mlinzi wa Haki za Binadamu dhidi ya ukiukwaji wa sheria na kanuni za nchi.
Baadhi ya wananchi wamekipongeza kituo cha ITV kwa kuwa mstari wa mbele kuielimisha jamiin ya Watanzania nchini kwa kuita watu mbalimbali kituoni hapo ili kuzungumzia masuala mbalimbali ambayo yana faida kwao na wamevitaka vituo vingine viige mfano huu ili Taifa letu liendelee kuidumisha Amani yetu kuiweka nchi katika utulivu na usalama.

Mwenyekiti wa TAMRA Bwana Belensi Alkadi akisikiliza mafunzo ya utetezi wa Haki za Binadamu katika Hotel ya White Sands Resort jijini Dar Es Salaam


 

Katibu Mkuu wa TAMRA Bwana Antony Sollo wa kwanza kushoto akiwa na baadhi ya wanasheria wa Chama cha kutetea Haki za Wanaume katika Hotel ya White Sands Resort Jijini Dar Es Salaam


 
Mwanasheria wa TAMRA Bwana Ben Shebakaki akiwa katika mafunzo ya utetezi wa Haki za Binadamu yaliyofanyika katika Hotel ya White Sands Resort jijini Dar Es Salaam




No comments:

Post a Comment