Wednesday, January 16, 2013

IMF YAKAMILISHA MAPITIO YA UTENDAJI



Bodi ya utendaji ya shirika la fedha la kimataifa IMF imekamilisha mapitio ya tano ya utendaji wa uchumi wa Tanzania na mapitio ya kwanza chini ya mpango wa msaada wa tahadhari
Akizungumza jijini Dar es salaam Waziri wa fedha Dk.William Mgimwa amesema badi hiyo pia imeridhia ombi la serikali ya Tanzania la kupewa msamaha wa kukiuka kigezo cha madeni ya nje yenye masharti ya kibiashara

Waziri Mgimwa amesema bodi hiyo pia imeridhishwa na mikakati iliyomo kwenye bajeti ya mwaka 2012/2013 ambayo amesema inazingatia uwiano mzuri baina ya matumizi ya maendeleo na matumizi katika huduma muhimu za kijamii
Waziri huyo amesema katika mpango huo Tanzania itanufaika na mkopo wenye masharti nafuu toka IMF wenye thamani ya dola za Marekani milioni 114

No comments:

Post a Comment