Thursday, January 17, 2013

TCRA YAFANYA KONGAMANO YA GHARAMA ZA MAKAMPUNI YA SIMU

Mamlaka ya mawasiliano nchini imefanya kongamano leo jijini Dar es Salaam juu ya gharama zinazotozwa na makampuni ya simu nchini
Mkutano huo uliojumusha watu mbalimbali kujadili gharama zitozwazo na makampuni ya simu Tanzania umefanyika na kuwapa watanzania ndani na nje ya Tanzania kujadili juu ya Gharama hizo
Maoni mengi ya watu hao yamesema kuwa gharama hizo ni kubwa sana na serikali inapaswa kusimamia makampuni hayo ili wawe na bei za kumuwezesha mtanzania yeyote kukidhi gharama hizo za simu kwa maana kupiga kwenda mtandao mwingine ni gharama sana.
Maoni hayo ya watanzania yanatazamiwa kuleta mabadiliko katika gharama hizo endapo serikali italisimamia hili

No comments:

Post a Comment