Wednesday, January 16, 2013

KIKWETE ATEMA CHECHE



Rais Jakaya Mrisho Kikwete amekemea tabia ya baadhi ya viongozi wa kisiasa kutumia suala la raslimali za taifa, ikiwamo gesi asilia kujifatufia umaarufu wa kisiasa na kuwapotosha wananchi.

Rais Kikwete ameyasema hayo wakati alipokutana na Balozi wa Uingereza nchini ambaye anamaliza muda wake, Dianne Corner  ambaye alifika Ikulu, Dar Es Salaam kumuaga

Rais Kikwete amesema kuwa ni jambo la hatari na lisilo na tija kwa wanasiasa kujaribu kuigawa nchi vipande vipande kwa sababu ya kujitafutia umaarufu kwa kutumia raslimali za taifa.


Balozi  Corner ambaye amekuwa Balozi wa Uingereza nchini Tanzania kwa miaka minne amehamishiwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Wakati huo huo Rais Kikwete usiku wa leo atampokea Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) na Rais wa Benin, Boni Yayi

Rais Yayi anawasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambapo mara baada ya kuwasili viongozi hao wawili watafanya mazungumzo kuhusu masuala mbali mbali yanayolihusu Bara la Afrika

No comments:

Post a Comment